Umuhimu wa miti

Kwa nini tunahitaji miti? Miti ni muhimu kwa wanadamu, wanyama na mazingira kwa jumla. Katika nakala hii tumekupa umuhimu wa miti katika sayari yetu.

Faida 10 za miti

  1. Miti ni makazi muhimu kwa wanyamapori
  2. Miti inaboresha ubora wa udongo
  3. Miti Inazuia mmomonyoko wa udongo
  4. Miti Kama chanzo cha chakula
  5. Miti husaidia katika kuzuia ukame
  6. Miti husaidia katika kuzuia ukame
  7. Miti hutoa nafasi za kazi
  8. Miti huhifadhi hewa
  9. Kwa makazi na kivuli
  10. Kuzuia mafuriko

Umuhimu wa miti

Miti ni makazi muhimu kwa wanyamapori

Aina mbalimbali za ndege, wadudu n.k. huishi katika makazi ya misitu. Viumbe hawa wamezoea mazingira yao kwa karne nyingi na wanaitegemea miti.

Wanyama wakubwa kama vile, twiga, tembo, pundamilia n.k. huishi kenye misitu na ukula baadhi ya miti kama chakula. Maelfu zaidi ya viumbe kama vile nyoka, vyura, mchwa, buibui, mende, nondo – wote hutegemea usalama wa miti na hufanya kama makazi.

Miti inaboresha ubora wa udongo

Miti ina jukumu muhimu sana katika kuboresha ubora wa udongo. Miti ina uwezo wa wa kuchuja kaboni, kwa hivyo, huondoa kaboni na vitu vingine vya sumu kutoka kwa udongo, na kuruhusu mimea mingine kustawi.

Miti huchangia madini muhimu kwa udongo kwa kumwaga majani yake yanayooza na kuwa rutuba muhimu.

Miti pia huboresha ubora wa udongo kwa kuvuta rutuba kutoka chini kabisa ya ardhi hadi juu ya ardhi kupitia mizizi yake. Hii inafanya udongo kuwa na lishe zaidi kwa mimea mingine.

Miti Inazuia mmomonyoko wa udongo

Kwa kutumia vigogo na majani, miti huunda kizuizi cha asili kwa upepo na mafuriko. Kizuizi hiki hupunguza nguvu ya maji na upepo na husaidia kuzuia udongo kuchukuliwa.

Mizizi ya miti pia hufanya kazi muhimu katika kushikilia udongo Pamoja na kuzuia mmomonyoko wa udongo. Katika maeneo yaliyokatwa miti, hakuna kitu cha kusikilia udongo pamoja au kupunguza kasi ya upepo. Kwa hivyo katika kipindi cha upepo mkali au mvua kali udongo wote uliolegea unachukuliwa, na kugeuza eneo hilo kuwa jangwa.

Miti Kama chanzo cha chakula

Kutoka kwa majani hadi matunda, syrup zinazoundwa kutoka kwa miti na viungo mbalimbali vilivyotengenezwa kutoka miti kama vile mdalasini. Miti ni chanzo cha muhimu cha chakula kwa wanadamu. Wanyama pia hutegemea matunda na majani ya miti kama chanzo chao cha chakula.

Miti husaidia katika kuzuia ukame

Mfumo wa mizizi ya mti huwajibika kwa ufyonzaji wa virutubisho na maji, kwa kutumia mizizi kama vitambuzi kutambua hali ya upungufu wa maji na kutuma ishara kwenye chipukizi juu ya ardhi. Spishi za asili zinazostahimili ukame zina mizizi inayotafuta maji ambayo hupenya ndani kabisa ya udongo ili kupenyeza maji ya chini ya ardhi ili kuteka juu ya uso.

Miti hutoa nafasi za kazi

Matunda yaliyovunwa kutoka kwa miti yanaweza kuuzwa, hivyo kutoa mapato kwa watu wengine. Uvunaji Magogo ni sekta ya misitu inahusisha kusimamia, kuvuna, na kusindika miti kwa ajili ya mbao na bidhaa zingine zinazotokana na mitii. Sekta hii inaajiri wafanyakazi kadhaa, wakiwemo wakataji miti na wataalamu wa usafirishaji.

Miti huhifadhi hewa

Miti hufyonza harufu na gesi chafuzi na kuchuja chembechembe kutoka angani kwa kuzinasa kwenye majani na magome yake, kutokana nah ii tunakuwa na hewa safi ya kupumua.

Kwa makazi na kivuli

Katika joto la kiangazi, miti hutoa kivuli na makazi muhimu kwa wanadamu na wanyama. Miti hutoa kivuli kwa kuzuia jua kutofika ardhini. Hii inaweza kupunguza joto kwa kiasi kikubwa, na kuifanya iwe rahisi zaidi kwa watu na wanyama. Miti pia hutoa ulinzi dhidi ya upepo na mvua. Hii inaweza kuwa muhimu kwa kutulinda kutokana na uharibifu, haswa wakati wa dhoruba.

Kuzuia mafuriko

Miti imeonyeshwa kuwa muhimu kama ulinzi wa mafuriko pia. Miti ikiwa karibu na mito, hupunguza kwa kiasi kikubwa kiwango cha maji ya mvua yanayoingia kwenye mikondo ya maji. Hii inapunguza uwezekano wa mito kupasua kingo zake na kusababisha mafuriko maeneo ya tambarare.

One response to “Umuhimu wa miti”

Related Posts