Silabi na mifano

Silabi ni nini?

Silabi ni fungu la sauti linalotamkwa kwa pamoja kama fungu moja la sauti. Silabi inaweza kuwa na irabu moja au zaidi, au konsonanti moja au zaidi.

Silabi inaweza kuundwa na:

1. Irabu peke yake

Mifano:

Ua: U – a

Oa: O – a

2. konsonanti peke yake.

Mifano:

Mke: M – ke

Nje: N-  je

3. konsonanti+irabu

Mifano:

Baba: Ba – ba

Peleka: Pe – le – ka

4. konsonanti+ konsonanti/ kiyeyusho+irabu

Mifano:

Mbali: Mba – li

Fyata: Fya – ta

Lizwa: Li -zwa

5. konsonanti + konsonanti + kiyeyusho na irabu

Mifano:

Jengwa: Je – ngwa

Mbweha: Mbwe – ha

6. Kiyeyusho + irabu

Mifano:

Waya:  Wa – ya

Yale: Ya – le

7. silabi funge

Mifano:

Labda: Lab – da

Daftari: Daf – tari

Aina za silabi

Katika lugha ya kiswahili zipo aina kuu mbili za silabi.

Nazo ni:

Silabi wazi na silabi funge.

Silabi wazi

Silabi wazi ni ile yenye vokali na inayoishia kwa irabu. Na matamshi yake aghalabu hua ni ya kibantu.

Silabi wazi pia iko na aina zake:

1. Silabi Sahili

Hizi ni silabi ambazo huwa na irabu na konsonanti zikifuatana mtawalia.

Mfano:

baba, mama, kalamu, kula, lala n.k

2. Silabi mwambatano

Huwa na konsonanti mbili zinazotangulia irabu.

Mfano:

mwalimu, mtoto, mfawidhi, mwezi, mvua, mkate, ndoo nk.

3. Silabi changamano

Huwa na konsonanti tatu zinazotangulia irabu.

Mfano:

mpwa, mbwa, mbweha.

Silabi funge au mkopo

Hupatikana kwa maneno yasiyo na asili ya kibantu (kigeni).

Mfano:

Mufti, Sadakta, Daftari

Related Posts