Matumizi ya kikomo

Kikomo ni alama ya uakifishaji inayotumika mwisho wa sentensi. Inaonyesha kwamba sentensi imekamilika na kwamba msomaji anapaswa kuendelea na sentensi inayofuata.

Matumizi ya kikomo

a) Mwishoni mwa sentensi

Huonyesha mwisho wa sentensi.

Mfano

 Kioo kimevunjika.

Mtoto ameenda shule.

Mama amepika chakula.

Nitafika nyumbani mapema.

b) Kufupisha maneno.

Mfano

S.L.P. (Sanduku la posta)

Bw. (Bwana)

Mhe. (Mheshimiwa)

U.N.O. Y.C.S. Dkt. N.k.

c) Kuonyesha saa/ muda

Mfano

Misa ilianza saa 4.30 asubuhi.

Saa 12:00.

Tukutane 2.45 alasiri.

d) Katika hesabu, huonyesha isiyo nzima.

Mfano

Ukigawa tatu mara mbili utapata   1.5

10/100 =0.1

e) Kuonyesha senti katika pesa.

Mfano

Bei yake ni shilingi 12.50

Sh 100.00 (shilingi mia moja)

f) Katika kuonyesha kiwango cha kitu

Mfano

Kg 2.5 (kilo mbili na nusu)

L 5.0 (lita tano)

Related Posts