Jinsi ya kupika pilau

Pilau ni nini?

Pilau ni wali uliyotiwa ladha ya nyama na viungo na wakati mwingine kupikwa kwa mboga. Hapa kuna njia mbili rahisi jinsi ya kupika pilau.

Njia rahisi ya kupika pilau

Viungo (Ingredients)

  • Kitunguu
  • Kitunguu saumu (Garlic)
  • Tangawizi (Ginger)
  • Vijiko 2-3 vya Pilau Masala
  • Kilo nusu ya nyama
  • Nyanya nne
  • Vikombe 2 vya Mchele
  • Vikombe 3 vya maji
  • Chumvi kiasi
  • Mafuta ya kupikia  (vijiko 2-3)

Njia:

  1. Pasha mafuta kwenye sufuria, ongeza vitunguu na tangawizi. Acha hii ichemke juu ya moto wa kati hadi iwe kahawia.
  2. Koroga nyama na uweke kifuniko juu ya sufuria. Acha nyama iive kwa takriban dakika tatu (nyama iwe laini). Ikiwa nyama haijalainika pika kwa dakika chache zaidi.
  3. Ongeza pilau masala na chumvi huku ukikoroga ili kuhakikisha viungo vimesambaa vizuri. (Unaweza pia kuongeza maji kidogo ikiwa nyama yako ni kavu na imeshikamana na sufuria.)
  4. Ongeza nyanya na uendelea kukoroga. Ongeza maji kidogo na ufunike sufuria, acha ichemke hadi mchanganyiko wako ukuwe na mchuzi mnene.
  5. Ongeza wali uliooshwa na uchanganye vizuri. Ongeza vikombe 3 vya maji, funika na acha hii ichemke juu ya moto wa wastani kwa dakika chache kama tano hivi.
  6. Punguza moto na uruhusu wali uive ukiwa umefunikwa.Baada ya takriban dakika 5 ya kupika, koroga mchele kwa kutumia kijiko na ufunike. Rudia kukoroga mara moja au mbili zaidi ili kuhakikisha kwamba wali unaiva sawasawa na haushikani chini ya sufuria.
  7. Mchele unapaswa kupikwa hadi maji yote yameyeyuka.
  8. Baada ya maji kuiva pilau imekuwa tayari kuliwa na kachumbari.

Njia nyingine ya kupika pilau

Viungo (Ingredients)

  • Vikombe 2 vya mchele
  • Viazi 5
  • Kikombe ¼  mafuta ya mboga
  • Vitunguu mbili vyekundu
  • Kitunguu saumu
  • Vijiko 2 vya tangawizi iliyokatwa
  • Pilipili moja
  • Kijiko moja cha pilau masala
  • Vijiko 2 vya beef cubes
  • Kilo moja ya nyama ya ng’ombe
  • Nyanya 3 zilizokatwa
  • Vikombe 4 vya maji
  • Majani mbili ya bay
  • Chumvi kiasi

Maagizo

  1. Pasha sufuria kwenye moto wa kati. Ongeza mafuta na uache mafuta ichemke kwa sekunde chache.
  2. Ongeza vitunguu vilivyokatwa na kaanga mpaka vitunguu vianze kugeuka rangi.
  3. Ongeza kitunguu saumu, tangawizi, pilipili, na pika kwa dakika moja hivi.
  4. Ongeza nyama iliyokatwa, pilau masala, beef cubes, majani ya bay na chumvi. Pika hadi nyama iwe na rangi ya kahawia ukiikoroga mara kwa mara kama dakika 8 hadi 10.
  5. Ongeza nyanya zilizokatwa na upika kwa muda mpaka nyanya zitoa mchuzi mnene.
  6. Ongeza viazi na maji na uchemshea na kupika kwa dakika kumi.
  7. Ongeza mchele na ukoroge, kisha ufunike sufuria yako, ikiwa ni lazima punguza moto kwa kiwango cha chini na upika kwa muda wa dakika 20, mpaka mchele utakapokauka.
  8. Mara tu mchele umekauka, ondoa ufuniko na ukoroge kwa kijiko ili kuhakikisha kwamba viungo vyote vimechanganyika.
  9. Baada ya maji kuiva pilau imekuwa tayari kuliwa na kachumbari.
Related Posts