Shani na Bala: Safari ya Uchoyo

Posted by:

|

On:

|

hadithi za Kiswahili

Habari za safari hii inamhusu Daudi, mtu mwema aliyependa wanyama wake kama familia. Siku moja, Daudi aliamua kubeba mizigo na punda wake wawili, Shani na Bala, kwenye safari ya kutafuta mashamba bora. Shani aliweka kichwa chake chini akitembea kwa bidii, huku Bala akienda kwa majivuno akitibutia kichwa chake kana kwamba yeye ndiye bosi.

Walitembea kwenye ardhi laini kwa masaa mengi, wakipita mashamba yenye matunda ya rangi kama dhahabu na miti mirefu inayochanza anga. Shani hakuwahi kulalamika, akivumilia jua kali na vumbi kwenye njia. Lakini kadri walivyokaribia milima, ardhi likaanza kubadilika. Njia ikawa ngumu, yenye mawe mengi na miteremko mikali.

Shani akaanza kupumua kwa shida, miguu yake ikitetemeka kutokana na kulemewa na uzito alioubeba. Akamgeukia Bala akimsihi kwa macho yenye huzuni, “Ndugu yangu, tafadhali punguza baadhi ya mizigo yangu. Nimechoka sana, naogopa nitaanguka.”

Bala akamtazama kwa dharau, na kumwambia, “Hapana! Mimi nimebeba sehemu yangu, wewe beba yako!”

Shani akaendelea kupambana, lakini mwili wake ukawa dhaifu sana. Akapoteza nguvu, akajikwaa na kuanguka kwenye mteremko wa mlima, mwili wake ukigonga miamba kwa sauti kali. Hakutoka pumzi tena. Daudi alichomwa na huzuni, machozi yakimtiririka usoni.

Lakini hakukuwa muda wa kuomboleza. Daudi akaongeza mizigo ya Shani kwa Bala, kisha akamtoa shani ngozi na kuweka juu ya mizigo. Bala aliweza kubeba uzito huo mwingi kwa shida tu, akilalamika kama mtoto mdogo ambaye pipi yake imechukuliwa.

Huku akitembea kwa taabu, Bala akaanza kunong’ona, “Nina adhabu yangu ninastahili tu. Kama ningemsaidia Shani mwanzoni, nisingekuwa ninabeba mzigo wake na ngozi yake sasa.”