Kinyume cha neno kali

Posted by:

|

On:

|

Kali ni:

-enye ubapa ulionolewa na unaoweza kukata kitu, -liochongoka.

Mfano: Shoka limenolewa na sasa ni kali.

-enye kupenda kudhuru kwa mfano kuuma, kukaripia na kadhalika.

-enye ladha kama pilipili iwapo mdomoni.

-enye kucheneta mwilini.

Mfano: Jangwani huwa na baridi kali.

Kinyume cha kali

Kinyume cha kali hutegemea ufafanuzi wa hapo juu:

Kinyume cha kali (-enye ubapa ulionolewa) ni butu.

Butu ni:

-siyokuwa na makali.

-siyokata.

Kinyume cha kali (-enye ladha kama pilipili) ni tamu.

Tamu ni -enye ladha ya kupendeza kinywani.

Kinyume cha kali (-enye kupenda kudhuru.) ni rahisi, laini, nyoofu au mpole.

Rahisi ni: sio ghali au sio ngumu.

Laini ni siyo ngumu au siokwaruza.

Kinyume cha kali (-enye kucheneta mwilini) ni nyepesi au tulivu.