Kinyume cha neno mtumwa

Posted by:

|

On:

|

Mtumwa ni mtu ambaye anamilikiwa na mtu mwingine na anayefanyishwa kazi bila malipo.

Kisawe cha mtumwa ni hadimu.

Kinyume cha mtumwa

Kinyume cha mtumwa ni: Mfalme, bwana, mwajiri, mnyapara, bosi, nk.

Mnyapara ni mtu anayesimamia kazi ili kuhakikisha kuwa inafanywa kama inavyotakiwa.

Mfalme ni mtawala ambaye apataye mamlaka ya kutawala kwa kumrithi mzazi wake.

Bosi ni mtu mkuu na mwenye madaraka katika ofisi au kazi fulani. Au mtu anayewapa watu ajira.

Mwajiri ni serikali, shirika au mtu binafsi anayempatia mtu kazi kwa mshahara.