Maana ya neno ach.a na English translation

Maana ya neno ach.a

1. (Kitenzi) <ele> sita kufanya jambo.

Mfano: Juma ameacha shule.

2. telekeza.

Mfano: Aliwaacha watoto wake nyumbani bila ya chakula.

3. toa maelekezo kuhusu jambo la kufanywa na mtu mwingine wakati unapoondoka mahali.

Mfano: Nilipokwenda kwake sikumkuta lakini niliacha ujumbe. 4. bakiza kitu. Kisawe chake ni saza.

Mfano: Mgeni ameacha chakula kingi.

5. -pa mwanamke talaka, kinyume chake ni taliki.

Mfano: Amemwacha mke wake.

6. ruhusu jambo lifanyike.

Mfano: Si vizuri kumwacha mtoto afanye apendavyo.

7. ondokana na tabia fulani. Kisawe chake ni koma.

Mfano: Acha kuvuta sigara. (nah) acha mkono fariki: Rafiki yetu ametuacha mkono.

Mnyambuliko wa neno acha ni: Achana, achika, achisha, achwa.

Ach.a Katika Kiingereza (English translation)

Ach.a katika Kiingereza ni inategemea na maana unayokusudia:

1. To stop, cease.

2. To leave, abandon, or forsake.

3. To give instructions to someone before leaving. (instruct, direct)

4. To leave something behind. (abandon, forsake)

5. To divorce a woman.

6. To allow something to happen. (permit, authorize)

7. To stop doing something.

Related Posts