Maana ya neno ada na English translation

Maana ya neno ada

1. (Nomino katika ngeli ya [i-/zi-]), gharama au karo anayolipa mtu ili apatiwe huduma fulani k.m. katika elimu, burudani au kupata uanachama katika chama

2. mila au desturi za jamii fulani.

Mfano: Kila kabila lina ada zake za maziko.

3. kawaida katika kufanya jambo.

Mfano: Kunywa chai kila jioni ni ada kwake.

(Methali) Ada ya mja hunena, muungwana ni kitendo.

Ada Katika Kiingereza (English translation)

Ada katika Kiingereza inategemea muktadha:

Ada ya gharama au karo ni: Fee, charge.

Ada ya mila na desturi ni: Culture, tradition.

Ada ya kawaida ni: Habit.

Related Posts