Maana ya neno aga na English translation

Maana ya neno aga

Matamshi: /aga/

Aga 1

(Kitenzi)

Maana: punga mkono au sema maneno ya kuashiria kuwa unaondoka.

(Msemo) Aga dunia: kufa, fariki dunia, kata roho.

Mnyambuliko wa neno aga ni: → agia, agika, agisha, agiwa, agwa.

Aga 2

(Kitenzi elekezi)

Maana: funga ukurasa uliokuwa umefunguliwa kwenye tarakilishi. Mnyambuliko wake ni: → agia, agika, agisha, agiwa.

Aga Katika Kiingereza (English translation)

Aga katika Kiingereza inategemea maana unayokusudia:

Aga ya kuashiria kuwa unaondoka ni: to wave goodbye, to bid farewell.

Aga ya funga ukurasa kwa tarakilishi ni: close or exit.

Related Posts