Maana ya neno akiba na English translation

Maana ya neno akiba

Matamshi: /akiba/

Akiba 1

(Nomino katika ngeli ya [i-zi])

Maana: hifadhi inayowekwa kwa matumizi ya baadaye.

Mfano: Hamisi amejifungulia akaunti ya akiba kwa ajili ya siku za uzeeni.

Methali: Akiba haiozi: Unachokihifadhi leo kitakufaa kesho.

Akiba 2

(Nomino katika ngeli ya [i-zi])

Maana: programu kwenye tarakilishi ambayo ni hifadhi badala ya data.

Akiba Katika Kiingereza (English translation)

Akiba katika KIingereza inategemea na maana unayokusudia:

  • Akiba (hifadhi inayowekwa kwa matumizi ya baadaye.) ni: Savings.
  • Akiba (programu kwenye tarakilishi ambayo ni hifadhi badala ya data.) ni: Data backup program.
Related Posts