Maana ya neno akisi na English translation

Maana ya neno akisi

Matamshi /akisi/

Akisi 1

(Kitenzi elekezi)

Maana: dunda kwa miale au mionzi ya mwanga mahali kama vile uso wa kioo au sura ya maji baharini, mtoni na ziwani.

(Mfano): Kioo changu kimezeeka; hakiakisi tena vizuri.

Mnyambuliko wake ni: → akisia, akisiana, akisika, akisisha, akisiwa.

Akisi 2

(Kitenzi elekezi)

Maana: toa ishara ya jambo fulani.

Mnyambuliko wake ni : → akisia, akisiana, akisika, akisisha, akisiwa.

Akisi 3

(Kitenzi elekezi)

Maana: lipa deni polepole katika muda mwafaka.

Akisi Katika Kiingereza (English translation)

Akisi katika KIingereza inategemea na maana unayokusudia:

  • Akisi (dunda kwa miale au mionzi ya mwanga mahali kama vile uso wa kioo au sura ya maji) ni: Reflection.
  • Akisi (toa ishara ya jambo fulani) ni: to show.
  • Akisi (lipa deni polepole katika muda mwafaka) ni: to pay off a debt in installments.
Related Posts