Maana ya neno alama na English translation

Maana ya neno alama

Matamshi: /alama/

Alama1

(Nomino katika ngeli ya [i-zi])

Maana: doa linalochafua kitu kama vile nguo, meza n.k.

Alama 2

(Nomino katika ngeli ya [i-zi])

1. maksi anazopewa mtu baada ya kufanya mtihani au katika shindano.

2. kitambulisho kama vile cha maandishi elekezi barabarani au umbo la nyayo za wanyama msituni.

Alama 3

(Nomino katika ngeli ya [i-zi])

Maana: ishara ya uakifishaji.

Alama Katika Kiingereza (English translation)

Alama katika Kiingereza inategemea na maana unayokusudia:

  • Alama (linalochafua kitu) ni: stain, mark.
  • Alama (maksi anazopewa mtu) ni: grade, score, marks.
  • Alama (ishara ya uakifishaji) ni: punctuation mark.
Related Posts