Maana ya neno amini na English translation

Posted by:

|

On:

|

Maana ya neno amini

Matamshi: /amini/

Amini 1

(Kitenzi elekezi)

Maana:

1. sadiki au kubalia ukweli wa kitu au jambo.

2. kubali kuwa fulani anakubalika.

Mfano: Juma hakuniangusha tamashani ndiyo maana ninamuamini.

Mnyambuliko wa amini ni: → aminia, aminiana, aminika, aminisha, aminiwa.

Amini 2

(Kitenzi elekezi)

Maana: sadiki na tekeleza mafunzo ya dini.

Mfano: Dini kuu duniani zinaamini kuwa Mungu ni mmoja.

Mnyambuliko wake ni: → aminia, aminiana, aminika, aminisha, aminiwa.

Amini Katika Kiingereza (English translation)

Amini katika Kiingereza inategemea na maana unayokusudia:

  • Amini (sadiki au kubalia ukweli wa kitu au jambo) ni: believe or accept the truth of something.
  • Amini (kubali kuwa fulani anakubalika) ni: trust.
  • Amini (sadiki na tekeleza mafunzo ya dini) ni: faith or religious adherence.