Methali 50 za bidii

Posted by:

|

On:

|

Hapa kuna methali 50 zinazozungumzia kufanya kazi kwa bidii. Kutokana na hizi methali utapata motisha ya kufanya kazi kwa bidii ili ufanikiwe.

Methali za bidii

  • Ajizi ni nyumba ya njaa

Methali hii inamaanisha uvivu unafanya mtu kuishi kwa umaskini.

  • Aisyekubali kushindwa si mshindani

Methali hii inamaanisha kwamba katika maisha kuna kupata na kukosa.

  • Atangaye na jua hujua

Methali hii inamaanisha kwamba anayejibidiisha na kutafuta hupata.

  • Baada ya dhiki faraja

Methali hii inamaanisha kwamba baada ya mateso utapata furaha.

  • Bahati ya mwenzio usiilalie mlango wazi

Methali hii ina maana kwamba kila mtu ana bahati yake.

  • Bandu bandu humaliza gogo

Methali hii inamaanisha kwamba kufanya kitu kidogo kidogo hatimaye humaliza kazi kubwa.

  • Bura yangu sibadili kwa Rehani

Methali hii ina maana kwamba usitupe kitu chako, hata kama ni kibaya, ukitamani cha mwenzio.

  • Chanda chema huvikwa pete

Methali hii ina maana kwamba anayefanya mema atatuzwa.

  • Chelewa chelewa, utakuta mwana si wako

Methali hii inamaanisha kwamba anayekuwa wa kwanza, hupata mambo mazuri.

  • Chovya chovya humaliza buyu laa asali

Methali hii ina maana kwamba kufanya jambo kidogokidogo, humaliza jambo zima.

  • Chungu kidogo huchemka upesi

Methali hii ina maana kwamba heri kufanya mambo madogo kwa haraka, kuliko mambo mengi kwa muda mrefu.

  • Chururu si ndondo

Methali hii ina maana kwamba heri kupata vitu vidogo vya kudumu kuliko vingi mara moja.

  • Debe shinda haliachi kutika

Methali hii inamaanisha kuwa wengi sana hupenda kusema bila kuonyesha utendaji.

  • Kazi mbi si mchezo mwema

Methali hii ina maana kwamba Kazi ngumu haina raha.

  • Kulea mimba si kazi kazi kulea mwana

Methali hii ina maana kwmaba kulea mtoto ni kazi ngumu kuliko kubeba mimba.

  • Kuvua si kazi kazi ni magawioni

Methali hii ina maana kwamba kazi halisi ni kupata samaki, sio kuvua.

  • Mume ni kazi mke ni nguo

Kazi hii ina maana kwamba mume ni jukumu, mke ni raha.

  • Mzoea udalali hawezi kazi ya duka

Methali hii ina maana kwamba mtu aliyezoea kazi moja hawezi kufanya kazi nyingine kirahisi.

  • Eda ni ada yenye faida

Methali hii ina maana kwamba uvumilivu na busara mara nyingi humnufaisha mwanadamu.

  • Fahari isiyo na ari haina heri

Methali hii ina maana kwamba utukufu hauwezi kuja bila kufanya kazi.

  • Fimbo ya mbali haiui nyoka

Methali hii ina maana kwamba kitu kilicho mbali hakiwezi kukupa msaada wa haraka.

  • Haba na haba hujaza kibaba.

Methali hii ina maana kwamba usidharau mambo madogo madogo kwa kuwa hayo ndiyo huishia kuwa makubwa baadaye.

  • Hakuna ziada mbovu

Methali hii inamaanisha kuwa chochote mtu apatacho chafaa.

  • Hatua moja hufupisha safari.

Methali hii inamaanisha kwamba hatua moja anayopiga binadamu anapotembea husaidia kufupisha mwendo.

  • Heri kwaa ya dole kuliko kwaa ya ulimi

Methali hii ina maana kwamba afadhali kukosea katika kutembea ukaumia kuliko kutamka maneno yatakayosababisha mgogoro.

  • Debe tupu haliachi kuvuma

Methali hii ina maana kwamba hata kitu kisicho na thamani kinazungumziwa sana.

  • Heri nusu shari kuliko shari kamili

Methali hii ina maana kwamba ni bora kupata matokeo mabaya kidogo kutopata hata kitu.

  • Subira yavuta heri na huleta kilicho mbali

Methali hii ina maana kwamba subira huleta matokeo mazuri.

  • Heri kujikwaa kidole kuliko ulimi

Hii methali inamaanisha kuwa ni bora kufanya makosa madogo kuliko makubwa.

  • Kila ndege huruka kwa ubawa wake

Methali hii ina maana kwamba kila mtu hufanya kazi au kufanya shughuli zake kulingana na uwezo wake.

  • Kitegwacho kukitega kwataka ubongo

Methali hii ina maana kwamba kazi yoyote inahitaji akili na ujuzi ili kuitekeleza.

  • Kula kutamu kulima mavune

Methali hii ina maana kwamba watu hupenda kufaidi bila kujihangaisha.

  • Kula uhondo kwataka matendo

Methali hii inamaanisha kuwa ili tuwe na maisha mema sharti tufanye kazi kwa bidi.

  • Kuzima koleo si mwisho wa uhunzi

Methali hii ina maana kwamba kupumzika siyo kuacha kazi.

  • Kwa mwoga huenda kicheko, kwa shujaa huenda kilio

Methali hii ina maana kuwa usipambane na jambo usiloliweza.

  • Maisha ni bahati ifumbate

Methali hii inamaanisha kuwa uhai ni majaaliwa utumie vizuri, maisha ni vita pigana ili uishi ni sharti uhangaike.

  • Mali bila daftari hupotea bila habari

Methali hii inamaanisha utunzaji wa kitu kwa umakini unahitaji uwekaji mzuri wa kumbukumbu.

  • Mbio za sakafuni huishia ukingoni

Methali hii inamaanisha jambo lenye mwanzo lazima liwe na mwisho, kwenda mbio sio kufika, kufanya jambo kwa haraka kunaweza kusiwe na matokeo mazuri.

  • Mchagua jembe si mkulima

Methali hii ina maana kuwa mwenye nia ya dhati hachagui kitendea kazi mtu mvivu husingizia vitendea kazi.

  • Mchele mmoja mapishi mbalimbali

Methali hii ina maana kuwa jambo moja linaweza kufanywa kwa namna mbalimbali.

  • Mchelea bahari si msafiri

Methali hii ina maana kuwa anayeiogopa bahari, hawezi kusafiri majini.

  • Mcheza hawi kiwete ngoma yataka matao

Methali hii ina maana kuwa kila shughuli anayoifanya binadamu inapaswa kufanywa kwa bidii na kujituma kwingi.

  • Mfa maji haishi kutapatapa

Methali hii ina maana kuwa mtu akipatwa na shida hutumia njia yoyote ili kujinusuru.

  • Mgaagaa na upwa, hali wali mkavu

Methali hii ina maana kuwa anayepita mahali penye riziki mara kwa mara aweza kubahatika.

  • Mkono mtupu haulambwi

Methali hii inamaanisha kuwa kama hauna kitu hutasaidika, lazima toa kitu ili upate kitu.

  • Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni

Hii methali ni kama mnyonge hana haki mpaka mwenye nguvu apende.

  • Mstahimilivu hula mbivu

Methali hii ina maana kuwa uvumilivu hadi mwisho unahitajika katika kufikia mema.

  • Mtaka cha mvunguni sharti ainame

Methali hii ina maana kuwa ili kupata mafanikio lazima kupitia misukosuko.

  • Mvumilivu hula mbivu

Methali hii ina maana kuwa mtu anayevumilia taabu na shida nyingi hupata mafaniko maishani.

  • Mwenda pole hajikwai

Methali hii ina maana kuwa ukifanya jambo kwa utaratibu utafanikiwa.

  • Mwenye nguvu mpishe

Methali hii ina maana kuwa si busara kupambana na mtu anayekuzidi uwezo.

  • Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu

Methali hii ina maana kuwa ni vizuri kushirikiana na binadamu wenzio.

  • Kula ni vyepesi lakini kulima ng’o

Methali ina maana kuwa kupata chakula ni rahisi kuliko kufanya kazi ili kupata chakula hicho.

Comments are closed.