Tashbihi ni lugha inayotumika kulinganisha vitu viwili vinavyofanana au kushabihiana. Inatumia viunganishi mithili ya, kama, mfano wa nk. Hii hap ani mifano ya tashbihi:
Mifano ya tashbihi
- Lala kama mfu
 - Ng’ara sawa kama mwezi
 - Mwoga mfano wa kunguru
 - Simama wima mithili ya dandalo
 - Ringa kama tausi
 - Lazima kama ibada
 - Mweusi mithili ya mkaa
 - Mrembo mithili ya Malaika
 - Cheka kama radi
 - Maridadi kama kipepeo
 - Nyeupe Kama theluji
 - Mfupi Kama nyundo
 - Mfupi kama mbilikimo
 - Mrefu Kama mlingoti
 - Mrefu kama ngamia
 - Mrefu kama twiga
 - Mweusi Kama makaa
 - Bahati kama mtende
 - Nukia kama ruhani
 - Nuka kama beberu
 - Tamu kama halua
 - Nzito kama nanga
 - Nyepesi kama unyoya
 - Majuto kama ya firauni
 - Kuiga kama kasuku.
 - Tumainia kama tai
 - Baridi kama barafu
 - Kigeugeu kama kinyonga
 - Mjanja Kama sungura
 - Pendana Kama chanda na pete
 - Tamu kama asali
 - Kali kama Shubiri
 - Tengana kama ardhi Na mbingu
 - Mnene kama nguruwe
 - Pendana kama ulimi na mate
 - Polepole kama kobe
 - Mweusi kama kizimwili
 - Fuata mtu mfano wa kondoo
 - Garagara kama mgonjwa
 - Kuwa na hakika kama mauti
 - Nata kama gundi
 - Kuwa imara kama mwamba
 - Mlafi kama fisi
 - Mwaminifu kama njiwa
 - Mjinga kama kondoo
 - Mwenye bidii kama mchwa
 - Mzima kama kigongo
 - Tumbo kama kuruba
 - Mkaidi kama punda
 - Mkaidi kama kirongwe
 - Laini kama hariri
 - Laini kama pamba
 - Mvumilivu kama mtumwa
 - Ganda kama kigaga
 - Msiri kama kaburi
 - Msiri kama kobe
 - Msiri kama usiku
 - Msiri kama mvaa buibui
 - Nata kama gundi
 - Mwembamba kama ufito
 - Mwembamba kama Uzi
 - Mropokaji kama mlevi
 - Baidika kama mbingu na ardhi
 - Shabihiana kama kurwa na Doro
 - Kigeugeu kama lumbwi
 - Mnafiki kama panya
 - Kung’aa kama dhahabu
 - Angaza kama jua
 - Laini kama hariri
 - Tamu kama asali
 - Nyeusi kama usiku wa manane
 - Mrembo kama Malaika
 - Jasiri kama simba
 - Akili kama mchwa
 - Chafu kama fugo
 - Cheka kama malaika
 - Chanua kama ua la asubuhi
 - Chungwa kama mfungwa
 - Dahadari kama anayekata roho
 - Mwenye bashasha kama mapambazuko
 - Mwenye bidii kama mchwa, nyuki
 - Mwenye nguvu kama tembo
 - Nyingi kama mchanga ufuoni
 - Mkali kama simbabuka
 - Mwenye maneno mengi kama chiriku
 - Tulia kama maji mtungini
 - Hasira kama za mkizi
 - Fuatana kama kumbikumbi
 - Sauti nzuri kama kinanda
 - Kuzurura kama mbwakoko
 - Kutapatapa kama samaki atolewapo majini
 - Mpofu kama jongoo
 - Tumbo kubwa kama kiriba.
 - Paa kama moshi
 - Maneno mengi kama chiriku
 - Imara kama chuma cha pua
 - Msahaulifu kama Nyati
 - Kupenda kama moyo
 - Wivu kama joka la mdimu
 - Mpole kama kondoo
 
One response to “Mifano 100 ya tashbihi”