Ngeli ya A-WA na mifano

Posted by:

|

On:

|

Hii ni ngeli ya majina ya viumbe wenye uhai kama vile watu, wanyama, ndege, wadudu, miungu, malaika n.k. Majina mengi katika ngeli ya A-WA huanza kwasauti M- kwa umoja na sauti WA- kwa wingi. Hatahivyo baadhi ya majina huchukua miundo tofauti.

Mifano ya nomino katika ngeli ya A – WA:

Wanadamu: mtoto, ndugu, msamaria, daktari, kiongozi

Wanyama: ng’ombe, mbuzi, swara, nyati, nguchiro

Ndege: bata, kuku, njiwa, mwewe, kipanga

Viumbe wa majini: samaki, papa, pweza, nyangumi na mamba

Wadudu: mende, mbu, kipepeo, nondo na nzi

Matakatifu wa kiimani: Mungu, Yesu, Mtume Mohammed na Malaika Israfili

Viumbe wasababishao zahama: jinni, pepo, na shatani

Mifano ya miundo ya ngeli ya A-WA;

KI-VI:  Kiwete—Viwete, Kipofu – Vipofu, Kijana – Vijana, Kifarau – Vifaru, Kipepeo – Vipepeo, Kibogoyo – Vibogoyo

M-MI: Mtume—Mitume, Mkunga – Mikunga, Mkizi – Mikizi

CH-VY: Chura—Vyura

MU-WA: Muungwana – Waangwana, Muuguzi – Wauguzi

MW-WA: Mwalimu-Walimu, Mwizi – Wezi

M-WA: Mtoto – Watoto, Mtu- Watu, Mkunga – Wakunga, Mwanamke – Wanawake, Mwanamume, Wanaume, Mgonjwa – Wangonjwa, Mchungaji – Wachungaji

Ꝋ-MA: Nabii – Manabii, Waziri-Mawaziri, Daktari – Madaktari

Ꝋ- Ꝋ: kuku-kuku, papa-papa, mbuzi-mbuzi, popo-popo, chui-chui

Mifano katika sentensi

Umoja: Mwalimu ndiye amemkataza kuingia.

Wingi: Walimu ndio wamemkataza kuingia.

Umoja: Kibogoyo amefika.

Wingi: Vibogoyo wamefika.

Umoja: Malaika alimtembelea nabii wa kale.

Wingi: Malaika walitembelea manabii wa kale.

Umoja: Ngombe anakula.

Wingi: Ngombe wanakula.

Umoja: Mbuzi alikimbia.

Wingi: Mbuzi walikimbia.

Umoja: Daktari alimtibu.

Wingi: Madaktari walimtibu.

Umoja: Mtoto alilia.

Wingi: Watoto walilia.

Umoja: Chura aliruka.

Wingi: Chura waliruka.

Comments are closed.