Ukubwa na udogo wa mtoto

Posted by:

|

On:

|

,

Mtoto ni:

  • Kiumbe mchanga anayezaliwa na mnyama au kiumbe yeyote mwenye uhai.
  • Mtu ambaye hajatimiza umri wa utu uzima.

Ukubwa wa mtoto.

Kupata ukubwa wa mtoto tunazingatia sheria hizi za ukubwa wa nomino:

Nomino zenye kiambishi {m} mwanzoni na zenye silabi moja katika mzizi, kiambishi hicho hudondoshwa na kupachikwa kiambishi {ji}. Neno mtoto hufuata sheria hii ingawa neno ‘mtoto’ lina angalau silabi mbili.

Nomino zilizo na kiambishi {m} mwanzoni na silabi mbili au zaidi katika mzizi, kiambishi hicho hudondoshwa. Neno mtoto linaaza na kiambishi {m}, na lina angalau silabi mbili.

Kufuata sheria hizi za ukubwa wa nomino, ukubwa wa mtoto ni: toto au jitoto.

Mfano

Mtoto analia. Ukubwa wake ni; Toto linalia au jitoto linalia.

Ukubwa wa mtoto, toto au jitoto, haya maneno yanachukua ngeli ya {li -ya}, katika sentensi. Kumaanisha {li} katika umoja na {ya} katika wingi. Na pia unapachika kiambishi {ma} kupata wingi wa toto.

Kwa mfano

Toto/jitoto linalia. Matoto/majitoto yanalia.

Mifano katika sentensi:

  • Toto hili linasumbua.
  • Jitoto hili linapenda kukula.
  • Alizaliwa akiwa jitoto kubwa sana.

Udogo wa mtoto.

Udogo wa mtoto ni kitoto ama kijitoto.

Mifano katika sentensi.

  • Kijitoto hiki ni kidogo sana.
  • Kitoto kinalia kwa sababu ya njaa.
  • Kitoto changu kina njaa.