Sala ya baba yetu uliye mbinguni (Lord’s prayer)

Posted by:

|

On:

|

Sala ya Bwana, pia inaitwa Baba Yetu, ni sala kuu ya Kikristo ambayo Yesu alifundisha kama njia ya kuomba. Sala ya Bwana katika biblia iko katika kitabu cha Mathayo 6:9-13 na Luka 11:2-4.

Sala ya Baba yetu

Hii hapa ni sala ya Baba yetu:

Baba yetu uliye mbinguni,

ina lako litukuzwe.

Ufalme wako uje,

Mapenzi yako yatimizwe

duniani, kama huko mbinguni.

Utupe leo mkate wetu wa kila siku,

na utusamehe makosa yetu,

kama sisi tunavyowasamehe waliotukosea.

wala usitutie majaribuni;

bali utuokoe na yule mwovu.

Amina.

Au

Baba yetu uliye mbinguni,

Jina lako litukuzwe;

Ufalme wako ufike,

Utakalo lifanyike

Duniani kama mbinguni.

Utupe leo mkate wetu wa kila siku,

Utusamehe makosa yetu,

Kama tunavyowasamehe waliotukosea.

Usitutie majaribu,

Lakini utuokoe na yule, muovu.

Amina.

Au

Baba yetu uliye mbinguni,

Jina lako litukuzwe,

Ufalme wako uje kwetu,

Mapenzi yako yatimizwe,

Duniani kama mbinguni.

Utupe leo mkate wetu wa kila siku.

Na utusamehe deni zetu,

Jinsi tunavyowasamehe wadeni wetu.

Wala usitutie majaribuni,

Bali utuokoe na yule mwovu.

Kwa maana ufalme ni wako,

na uweza, na utukufu, milele.

Amina.