Ney Wa Mitego: Sauti Ya Watu Lyrics na Jumbe Muhimu

Posted by:

|

On:

|

Hapa kuna Sauti Ya Watu Lyrics by Ney Wa Mitego. Mwishoni utapata ujumbe muhimu unaowasilishwa na wimbo huu.

Ney Wa Mitego: Sauti Ya Watu Lyrics

Hii sio sauti ya kiharakati, wala

Ukombozi wa musa na fimbo yake

Bali haya ni maumivu ya mnyonge

Anaye wakilisha walala hoi wenzake

Kwenye kinywa kilicho kosa

Pa kusemea hisia zake

Natanguliza samahani kwa wale nitakao wakwaza

Yamenifika hapa nimeshaidwa kunyamaza

Wapo wengi kama mimi wenye sauti kama mimi

Sijui ni ubinafsi hawasemi kama mimi

Anko alisema kwamba tuko uchumi wakati

Haya tudanganyeni tena tupo uchumi wa ngapi

Wapigaji waliotumbuliwa ndio wamerudi mzigoni

Kameadi ka million mnataja mabilioni damn

Amna huruma ninyi na sisi masikini

Hivi hio bajeti si mngeweka hospitalini

Na huyu ndio Yule binti aliemaliza chuo

Ila uakka wakazi aliyosomea uko chuo

Hajua atafanya nini amebaki na vyeti vyake

Anajuta alisoma nini si angejiuza ka wenzake

Panya road jina la pili la kijana asiekua na ajira

Na risasi ndio hukumu inamfika hata asie na hatia

Hakuna uafadhari wa maisha vyuma vimezidi kukaza

Mambo yanaharibika na wapinzani wamenyamaza

Kama ulimpenda baba huwezi mwelewa mama

Na kama hukumpеnda baba bado utamchukia mama

Yani kumpenda mama na kumchukia baba ni sawa

Kuipenda nyama halafu upendi mchuzi wakе

Mmmh, hii ni sauti ya watu

(Na hili giza tunaenda wapi

Tunafanya nini

Tutaishi vipi

Hata mwanga hauonekani)

Ukiona mtoto halii njaa na nyumbani hakuna chakula

We mchunguze vizuri kuna sehemu anakula

Mwambieni ukweli mama hali mbaya sio tandale sio masaki

Kilio cha kila mtu pesa hakuna imefichwa wapi

Siku hizi mpaka vigenge vya nyanya TRA wanataka kodi

Masikini amejichanga vipesa benki anakatwa tozo

Hizo V8 mnazonunua si hela zetu za kodi

Naona mna enjoy kuliko hata walipa kodi

Mnajenga hospitali madawa hakuna

Mnatujengea shule lakini walimu hatuna

Kudanga ndio kimbilio kubwa la dada zetu

Ndio mtaji asiokopeshwa hakatwi tozo wala kodi

Hivi mnaakili nyinyi mnashauri tujiajiri

Wakati nyinyi wenyewe mpaka sasa mmeajiriwa

Achieni nafasi zenu nanyinyi mkajiajiri

Hapo ndipo nitapoamini kweri nyie washauri wazuri

Kati ya mtawala na mpinzani hapa muogo nani

Mtawala aliekataza mikutano isifanyike

Au mpinzani asieifanya na anajua ni haki yake

Mmmh, hii ni sauti ya watu

(Na hili giza tunaenda wapi

Tunafanya nini

Tutaishi vipi

Hata mwanga hauonekani)

He he he

Bi mkubwa anapambana sana

Pengine hofu ni kuhusu swali la msingi kwenye vijiwe vyetu

Je vita yake na anaowaamini ni sawa

Zisije zikawa ni mbili tofauti

Tumerudi kule kule

Maji ya mgao umeme mgao

Maji hayatoki bili zinatoka

Mmmh, polisi hongereni kwa jitihada nyingi

Hamsemwi kwa ubaya lakini pia hamsingiziwi

Acha iendelee kunyesha tuone panapovuja

Jumbe za kujifunza kutoka kwa “Ney Wa Mitego: Sauti Ya Watu”

Maneno ya wimbo huu yanawasilisha ujumbe kadhaa, zikiwemo changamoto za kijamii na kiuchumi, mapambano ya watu wa kawaida, na wito wa uwajibikaji. Hapa kuna baadhi ya ujumbe uliotolewa kutoka kwa wimbo huu:

Mapambano ya kijamii na kiuchumi

“Hii sio sauti ya kiharakati, wala Ukombozi wa Musa na fimbo yake. Bali haya ni maumivu ya mnyonge, Anaye wakilisha walala hoi wenzake.”

Maneno haya yanaangazia mapambano na maumivu ya kila siku ya watu wasio na uwezo katika jamii, yakiwakilisha sauti ya waliokandamizwa.

Wito wa uwajibikaji na uwazi

“Wapigaji waliotumbuliwa ndio wamerudi mzigoni, Kameadi ka million mnataja mabilioni damn. Amna huruma ninyi na sisi masikini.”

Maneno haya yakosoa ufisadi na ukosefu wa huruma kwa maskini, yakitilia shaka mgao wa fedha na rasilimali.

Changamoto wanazokumbana nazo vijana

“Panya road jina la pili la kijana asiekua na ajira. Na risasi ndio hukumu inamfika hata asiye na hatia.”

Maneno haya yanazungumzia changamoto zinazowakabili vijana, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa ajira na matokeo mabaya wanayoweza kukabiliana nayo.

Ukosoaji wa kisiasa na maoni ya kijamii

“Kati ya mtawala na mpinzani hapa muogo nani. Mtawala aliekataza mikutano isifanyike. Au mpinzani asieifanya na anajua ni haki yake.”

Maneno hayo yanawakosoa watawala na viongozi wa upinzani, yakitilia shaka kujitolea kwao kwa maadili ya kidemokrasia na haki za raia.

Uwezeshaji na kujitegemea

“Hivi mnaakili nyinyi mnashauri tujiajiri. Wakati nyinyi wenyewe mpaka sasa mmeajiriwa.”

Maneno haya yanapinga ushauri wa kujiajiri wakati wale wanaotoa ushauri mara nyingi wameajiriwa wenyewe, wakitaka fursa za uwezeshaji za kweli.