Category: Maana ya maneno

  • Maana ya neno abee! na English translation

    Maana ya neno abee! (Kihisishi) neno la kuitikia wito litumiwalo na wanawake wanapoitwa. Visawe ni: bee, beka. Abee! Katika Kiingereza (English translation) Abee! Katika Kiingereza ni: Yes. Read more

  • Maana ya neno abedari na English translation

    Maana ya neno abedari 1. (Nomino katika ngeli ya [i-/zi-]) (bah) roda inayotumiwa kuvutia vitu kwenye jahazi. Kisawe ni kapi. 2. (Kielezi) neno la kumtahadharisha mtu. Visawe ni: simile!, kaa chonjo! Abedari Katika Kiingereza (English translation) Abedari katika Kiingereza hutegemea maana unayokusudia: Abedari inayovuta vitu kwenye jahazi ni: Pulley. Abedari ya kumtahadharisha mtu ni: Careful,… Read more

  • Maana ya neno abdi na English Translation

    Maana ya neno abdi (Nomino katika ngeli ya [a-/wa-]) (ush) mlimwengu, mja wa Mwenyezi Mungu. Kisawe chake ni abidi. Abdi Katika Kiingereza (English translation) Abdi katika Kiingereza ni: Worshipper, servant of God. Read more

  • Maana ya neno abakusi na English translation

    Maana ya neno abakusi (Nomino katika ngeli ya [i-/zi-]), kifaa chenye shanga au vihesabio vilivyotungwa kwenye nyuzi au nyaya kwa ajili ya kuhesabia. Abakusi Katika Kiingereza (English translation) Abakusi katika Kiingereza ni: Abacus. Read more

  • Maana ya neno abadi na English translation

    Maana ya neno abadi (Kielezi), neno linaloonyesha kutokoma kwa muda; daima, milele. Mfano: Anaishi hapa abadi. Abadi Katika Kiingereza (English translation) Abadi katika Kiingereza ni: Eternal. Read more

  • Maana ya neno abadani na English translation

    Maana ya neno abadani (Kitenzi) neno la kusisitiza jambo lililo- tajwa ambalo limekanushwa. Visawe ni: hata kidogo, katakata, kamwe, asilani, katu. Mfano: Sitakuja kwako abadani. Abadani Katika Kiingereza (English translation) Abadani katika Kiingereza ni: never. Read more

  • Maana ya neno abaa! na English translation

    Maana ya neno abaa! (Kihisishi) neno linalojenga usikivu wa yule unayemwita. Visawe ni: aisee, halo, oha. Abaa! Katika Kiingereza (English translation) Abaa! katika kiingereza linaweza tafsiriwa kama “Hey!” Read more

  • Maana ya aazi na English translation

    Maana ya aazi 1. (Nomino katika ngeli ya [a-/wa-]), ni mtu wa thamani. Visawe ni: mwa- ndani, muhibu. 2. (Kkivumishi) -enye thamani. Kisawe ni bora. Mfano: Fursa niliyopewa ni kitu aazi kwangu. Aazi Katika Kiingereza (English translation) Aazi katika Kiingereza ni: valuable, precious. Read more

  • Maana ya aathari na English translation

    Maana ya aathari Aathari ni nomino katika ngeli ya [i-/zi-], mabaki (yatokanayo) na vitu vya zamani vinavyohusiana na mila, utamaduni na desturi za watu wa jamii fulani. Mfano: makaburi ya wafalme, nyumba, mahekalu, vigae vya vitu vya ufinyanzi n.k. Aathari Katika Kiingereza (English translation) Aathari katika Kiingereza ni “historical remains.” Read more

  • Maana ya aalimu na English Translation

    Aalimu ni nomino katika ngeli ya  [a-/wa-] Wingi wa aalimu ni maalimu. Neno aalimu linatumika katika muktadha wa dini. Maana ya aalimu 1. Aalimu ni mtu aliye- bobea katika elimu dini ya Kiislamu. 2. (kama kivumishi) mwenye elimu kubwa ya dini ya Kiislamu. Aalimu Katika Kiingereza (English translation) Aalimu katika kiingereza anaweza tafsiriwa kama “Islamic… Read more