Mhariri Forum

Yesu kwetu ni rafik…
 
Notifications
Clear all

Yesu kwetu ni rafiki lyrics


(@kwamboka)
Trusted Member
Joined: 3 months ago
Posts: 31
Topic starter  

Yesu kwetu ni rafiki,

Haja zote hujua,

Tukiomba kwa Babaye

Maombi asikia,

Lakini twajikosesha,

Twajitweka vibaya,

Kwamba tukimwomba Mungu,

Dua atasikia.

Una dhiki na maonjo?

Una mashaka pia?

Haifai kufa moyo,

Dua atasikia.

Hakuna mwingine mwema

Wa kutuhurumia

Atujua tu dhaifu,

Maombi asikia.

Je, hunazo hata nguvu,

Huwezi  kwendelea?

Ujapodharauliwa,

Ujaporushwa pia,

Watu wangekudharau,

Wapendao dunia

Hukwambata mikononi,

Dua atasikia.

https://mhariri.com/song-lyrics/gospel-lyrics/yesu-kwetu-ni-rafiki-lyrics-na-mafunzo/


   
Quote