Mhariri Forum

Notifications
Clear all

Taja ngeli za kiswahili na mifano yake

   RSS

0
Topic starter

ngeli za kiswahili na mifano yake

4 Answers
0

Mifano ya nomino katika ngeli ya A – WA:

  • Wanadamu: mtoto, ndugu, msamaria, daktari, kiongozi
  • Wanyama: ng’ombe, mbuzi, swara, nyati, nguchiro
  • Ndege: bata, kuku, njiwa, mwewe, kipanga

Soma zaidi

0

Ngeli ya I-ZI

Haya ni majina ya vitu visivyokuwa na uhai .

Nomino katika ngeli hii huchukua I kwa umoja na ZI kwa wingi
Mifano ya nomino katika ngeli hii ni: Dawa, saa, ndizi, redio, ngoma, nyumba, chupa, radi na kadhalika.

Mifano katika sentensi.

1)Ngoma hii haipendezi (umoja). Ngoma hizi hazipendezi. (wingi)
2)Dawa hii inanidhuru (umoja). Dawa hizi zinadhuru (wingi)
3)Chupa imevunjika (umoja). Chupa zimevunjika (wingi)

NGELI YA U-ZI

Majina katika ngeli hii huhusisha vitu vyembamba na virefu ,yenye wingi wa ‘ny’ au ‘m’ au ‘nd’ ambayo yanatumia upatanisho wa kisarufi wa ‘u’.

Mifano ya majina katika ngeli hii:

1) Ukucha
2) Ulimi 
3) Ukuta 
4) waya 
5) Ufa
6) Ubawa 
7) Wimbo 
8) Wakati 

0

Mifano ya ngeli na mifano

Ngeli ya LI-YA

Inahusisha nomino zinazoanza kwa “Ji” katika umoja na “Ma” katika wingi.

Mifano:

Jino limeng’oka (Umoja) – Meno yameng’oka (Wingi)
Jicho limevimba (Umoja) – Macho yamevimba (Wingi)
Tunda limeoza (Umoja) – Matunda yameoza (Wingi)

Ngeli ya KI-VI

Ngeli ya KI-VI inatumiwa kuashiria hasa viumbe visivyo na uhai.

Mfano:

Kijiko «ki»mepotea.
Vijiko «vi»mepotea.

0

Mifano ya ngeli za Kiswahili:

Ngeli ya U-U

Mfano:

Ukaidi wake «u»limchongea.
Ukaidi wao «u»liwachongea.

Ngeli ya U-YA

Huwa na majina ya hali, matendo, na kadhalika. Kiambishi {–u} katika umoja na {–ya} katika wingi hutumika katika upatanisho wake wa kisarufi.

Mfano:

Upishi wake «u»mewavutia.
Mapishi yake «ya»mewavutia.

Ngeli ya YA – YA

Mfano:

Mafuta
Maarifa
Mazingaombwe
Maasi
Mamlaka
Makala n.k.