Mhariri Forum

Notifications
Clear all

Toa mifano ya vivumishi vya nomino

   RSS

0
Topic starter

mifano ya vivumishi vya nomino

4 Answers
0

Vivumishi ni vya aina kumi:
– Vivumishi vya sifa
– Vivumishi vya idadi
– Vivumishi visisitizi
– vivumishi vimilikishi
– Vivumishi virejeshi
– Vivumishi vionyeshi
– Vivumishi vya a- unganifu
– Vivumishi vya nomino kwa nomino.
– Vivumishi vya pekee
– Vivumishi viulizi

0

Mifano ya vivumishi

– Vivumishi vya sifa

Mfano: kizuri, kali, safi, mrembo
– Vivumishi vya idadi

Mfano: tatu, mbili, kumi, chache, nyingi, kadhaa, kidogo, wastani
– Vivumishi visisitizi

Mfano: yuyu huyu, wawa hawa, kiki hiki, papo hapo, mumu humu
– vivumishi vimilikishi

Mfano: changu, lako, yake, kwetu, vyenu, zao

– Vivumishi viulizi

Mfano: -ngapi?, -pi?

0

1. Vivumishi Visisitizi

Husisitiza nomino fulani kwa kurudia rudia 
k.m: 

  • Jahazi lili hili
  • Wembe ule ule
  • Ng’ombe wawa hawa

2. Vivumishi Viashiria / Vionyeshi

Vivumishi viashiria hutumika kuonyesha au kuashiria nomino kulingana na mahali.
Mfano: Karibu hapa, huyu, hiki, hili, huku, haya, ule, wale, pale, Mbali kidogo hapo, huyo, hiyo, hicho

0

Vivumishi visisitizi

Mfano: yuyu huyu, wawa hawa, kiki hiki, papo hapo, mumu humu

Vivumishi vimilikishi

Mfano: changu, lako, yake, kwetu, vyenu, zao