Mhariri Forum

Notifications
Clear all

Mifano katika ngeli ya PA/KU/MU

   RSS

0
Topic starter

ngeli ya PA/KU/MU

4 Answers
0

Ngeli hii, inayojulikana kama Ngeli ya Mahali, hufafanua matumizi ya viambishi “-pa-“, “-ku-“, na “-mu-” katika sarufi ya Kiswahili. Viambishi hivi hutumika kuonyesha mahali pa nomino.

Nomino zingine zinazoainishwa katika ngeli hii ni pamoja na “mahali” na “pahali.” Nomino za kawaida zinapoongezwa kiambishi tamati “-ni,” huainishwa katika Ngeli ya Mahali.

Mfano:

Usoni
Shuleni
Moyoni
Makundi Matatu ya Ngeli ya Mahali:

Ngeli ya Mahali imegawanywa katika makundi matatu makuu yanayoonyesha mahali maalum kwa mujibu wa nomino husika:

1. PA-PA:

Kundi hili linaonyesha mahali dhahiri, panapoonekana wazi.

Mfano:

Usoni pake pana tabasamu la daktari.
Nyusoni mwao pana tabasamu la daktari.
Kichwani pake pana kofia nyeupe.
Vichwani mwao pana kofia nyeupe.
2. KU-KU:

Kundi hili linaonyesha mahali kulikosiringirwa, mahali kusikodhihirika.

Mfano:

Shuleni kwangu kuna mwalimu stadi.
Shuleni kwetu kuna walimu stadi.
Uwanjani huko uendako kuna mchezo.
Nyanjani huko mwendako kuna michezo.
3. MU-MU:

Kundi hili linaonyesha mahali mlimo ndani, yaani undani wa kitu fulani.

Mfano:

Moyoni mwangu mna raha.
Mioyoni mwetu mna raha.
Garini humu mna mzigo mzito.
Magarini humu mna mizigo mizito.

0

PA (mahali karibu au panapodhihirika) k.m. Kitabu kipo pale.
KU (mahali mbali au kusikodhihirika) k.m. Mahali kule kunafaa.
MU (ndani ya) k.m. Mahali mle mna siafu.

0

Mfano wa majina katika hii ngeli ni: Hekaluni,msikitini,mahegeshoni,shimoni, mkobani, sebuleni, uwanjani, chumbani, darasani, kaburini, nk.

0

Mfano: shuleni, pangoni, jikoni, shambani nk