Mhariri Forum

Notifications
Clear all

Jinsi ya kuendelea baada ya kuachana na mtu?

   RSS

0
Topic starter

How to get over a breakup?

6 Answers
0

Jaribu kutomfikiria huyo mtu mpaka atoke kwa akili yako, na baada wa muda fulani utajipata umemsahau kabisa. Njia ingine ni kujizuia kumpigia simu ama kumtafuta kwa simu kwa njia yoyote.

0

Ukweli ni kuwa kujisikia vizuri baada ya kuachana na mtu huenda kutachukua muda. Unaweza hata kuenda mwaka mzima na maumivu ya kuachana na mpenzi wako, wakati mwingine unaweza kuwa na mlolongo wa siku nzuri bila kufikiria uhusiano wenu kabla ya kitu kukuchochea na kukurudisha pale ulipoanzia. Tambua kuwa ni kawaida, kupona hakufanyiki kila wakati. Inawezekana hata hautawahi kuwa bora mtu huyu. Hiyo ni kawaida pia. Jambo kuu ni kujifunza kuendelea maishani.

0

Jambo la kushangaza ni kwamba sababu mojawapo ya kutengana kuwa ngumu sana ni kwa sababu tunakosa kujitambua tulikuwa nani kabla ya kukutana na mtu huyo tumeachana naye. Utafiti unaonyesha kuwa talaka hupelekea wewe kukosa  kujitegemea. Unapopoteza uhusiano, sehemu ya jinsi ulivyo kama mtu huenda nayo. Kwa hivyo unapunguzaje pigo la talaka na kuachana? Itumie kama fursa ya kujitambua upya ujue wewe ni nani.

0

Ingawa ni jambo la kawaida kuchana na mtu na ni lazima ichukue muda kabla ya kujihisi kama wewe tena, kutokuwa sawa kadiri muda unavyosonga kunaweza kukutia wasiwasi. Kama siku nyingi zimepita na unatatizika kufanya kazi kazini au shuleni, tafadhali nenda ukazungumze na mtalaam

0

Tunapokumbuka mahusiano ya zamani, ni jambo la kawaida kukumbuka tu kumbukumbu za kupendeza, lakini kumtazama mpenzi wako wa zamani kwa njia hiyo hakufai na kutafanya iwe vigumu zaidi kuendelea. Baada ya kutengana, mara nyingi tunamfikiria mtu ambaye alivunja mioyo yetu au kutufanya tuwe na huzuni na kusahau mambo yoyote mabaya. Ukifikiria vile ulikuwa ukiteseka kwa uhusiano huo kutakusaidia kuendelee maishani.

0

Kubali hisia zako, jipe muda, zungumza na marafiki, epuka mawasiliano, jitunze, jifunze kutokana na uhusiano, pata usaidizi wa kitaalamu, tafakari malengo yako, usilazimishe mahusiano mapya, na kumbuka thamani yako.